Monday, August 13, 2012

Olympic 2012 yamalizika, Uganda na Kenya wachekelea. Tz tunajipangaje 2016?

Ugandan S. Kiprotch

Kutoka shoto Kirui (Silver), W. Kiprotchi (Bronze) na Ugandan S. Kiprotch (Gold)

Michezo ya Olympic kwa mwaka 2012 imemalizika jana huku majirani zetu wa Uganda na Kenya wakiwa wanachekelea kwa ushindi walioupata katika mbio za Marathon za wanaume za  kilomita 42.195 ambapo Mganda S. Kiprotich aliibuka na medali ya Dhahabu huku Wakenya Kirui na W. Kiprotich wakipata medali ya Silver na Bronze. Kwa kifupi matekeo yalikuwa hivi Gold: S.Kiprotich 2.08.01 Uganda ; Silver: Kirui 2.08.26 Kenya na Bronze: W.Kiprotich2.09.36 Kenya
Wakati majirani zetu wa Afrika Mashariki wakimaliza vizuri sisi mshiriki wetu kwenye mbio hizo F. Mussa alimaliza akiwa nafasi ya 33 na alitumia muda wa masaa 2.08.26 na Kaptain wa Team Samson Ramadhani alimaliza akiwa wa 66 kwa kutumia masaa 2.24.52.
Mitaa ya Kampla jana ilikuwa na shamrashamra nyingi kutokana na ushindi huo wa Gold medal ambao kwa mara ya mwisho walizweza kupata Gold medal miaka 40 iliyopita.
Nako Kenya, Serikali ya Kenya na wanachi wake kwa ujumla hawakufurahishwa na performance ya Timu yao nzima iliyokwenda London kwenye Olympic mwaka huu amabpo mpak awanamaliza wamepata Gold medal mbili tu. Kutokana na performance hiyo ilimlazima Waziri mkuu atembelee kambi yao huko London ili kuwapa moyo na kujua tatizo ni nini. Kwa kujitetea Viongozi wa Kenya Olympic Team wamedai kuwa kilichowagharimu ni kosa la wao kufanya mazoezi yaliyokuwa yakishuhudiwa na Wapinzani wao na kuweza kuibiwa techniques zao. Pia waliongeza kuwa hakukuwa na Team work kwenye timu yao. Waziri wa Michezo wa Kenya nae akiongea jnna baada ya mashindano hayo amesema Timu yao ya Olympic 2012 itaanza maandalizi rasmi miezi mine kuanzia sasa ili iweze kufanya vizuri mwaka 2012.
Je, Tanzania kutokana na hali halisi ya Team yetu na performance yetu tumejifunza nini? Tunajipanga vipi kwa ajili ya mwaka 2016?  Naipenda nchi yangu Tanzania na ninapenda sana siku moja na sisi turudi na medali kadhaa nyumbani. Kwahiyo muda wa maadalizi uwe na sasa na sio tusubibiri 2016!! Kila la Heri Tanzania kwa next Olympic games.

No comments:

Post a Comment