Friday, July 27, 2012

HAMIS KIIZA AIPELEKA YANGA FAINALI

Hamis Kiiza akishangilia na wachezaji wenzie wa Yanga baada ya kufunga goli la pekee jana

Mchezaji Hamis Kiiza ya Yanga mwenye asili ya Uganda jana amefanikiwa kuipeleka timu yake ya Dar Young African kwenye fainali ya kombe la Kagame kwa goli pekee alilofunga kwenye mchezo huo katika kipindi cha nyongeza. Kiiza alifunga bao hilo, kwa kichwa akiunganisha krosi ya karibu ya Haruna Niyonzima ambaye alitumia mwanya wa mabeki wa APR kuzubaa wakisikilizia maamuzi ya refa, baada ya Kiiza kuangushwa.
Yanga waliinuka na wakaanzisha shambulizi la haraka lililozaa bao hilo. Dakika tatu baada ya bao hilo, beki wa Yanga, Godfrey Taita alitolewa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja na sasa ataikosa fainali.
Katika Fainali hiyo ambayo intachezwa jumamosi katika uwanja wa Taifa Yanga watakutana na Azam Fm amabo wlaipata nafasi hiyo kwa kuitoa timu ya Simba SC kwa kipigo cha mabao 3-1 mwanzoni wiki hii. Mechi hii ambayo inatarajiwa kuwa katika mechi ngumu katika kombe hili ambapo watani wa jadi wa Yanga Simba wakiwa wanaombea watani wao wa Jadi kiwakute kile kilichowakuta wao kutoka kwa wababe hao Azam; wakati tiku ya Yanga yenyewe ikiwa na kazi mbili tofauti, moja ya kutetea kombe na ya pili kuonyesha kwamba hawako tayari kunywesha juice ya Vijoti kutoka kwa wana Azam Fc

Kikosi cha Yanga kitakachopambana Jumamosi

Kikosi cha Azamu kitakachopambana jumamosi
more pictures after the cut...
Mashabiki wa Yanga wakishangilia ushindi wao jana

Mashabiki wa Yanga wakishangilia ushindi wao jana

No comments:

Post a Comment