Showing posts with label Sport. Show all posts
Showing posts with label Sport. Show all posts

Tuesday, October 2, 2012

Kuelekea mechi ya wapinzani wa jadi... utani nao wazidi..


Hawa watani wa jadi na utani wao, ila majibu yote yatapatikana hapo kesho usiku ambapo wapinzani hao watakapochuana

Monday, October 1, 2012

Mashindano ya Kimataifa ya Mashua yafana DSM

Mshiriki wa mashindano ya Kimataifa ya mashua akijiandaa kuingia baharini tayari kwa kuyaanza mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ufukwe wa Yatch Club,Masaki jijini Dar.Mashindano hayo yalidhaminiwa na kampuni ya bia ya TBL kupitia bia yake ya Castle Lite.


Sehemu ya washiriki wa mashindano ya Kimataifa ya mashua wakijiandaa kuingia baharini tayari kwa kushindana,mashindano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki kwenye ufukwe wa Yatch Club,Masaki jijini Dar.Mashindano hayo yalidhaminiwa na kampuni ya bia ya TBL kupitia bia yake ya Castle Lite.


Washiriki wakichuana vikali katika mahsindano hayo

Washiriki wa mashindano ya Kimataifa ya mashua yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ufukwe wa Yatch Club,Masaki jijini Dar wakishindano katika kati ya bahari.Mashindano hayo yalidhaminiwa na kampuni ya bia ya TBL kupitia bia yake ya Castle Lite.


Washiriki wawkiendelea na mchuano

Thursday, September 20, 2012

Photo 2 of the day... ni raha tuu

Wachezaji wa SSC jana hiyo wakiwa na raha tele na huku wakimpongeza mchezaji mwenzao kwa kupachika goli.

Uwanja wa Taifa nako jana Mnyama aka Simba Sports club waliwapa raha mashabiki wao baada y aKumfunga JKT Ruvu 2-0. Magoli hayo yalifungwa na Amiri Kiemba na Haruna Moshi 'Boban'. Kwa sasa SSC ndio wako juu kwenye ligi hiyo bada ya pia kushinda mechi yao ya kwanza dhidi ya African Lyon ambapo SSC walishinda 3-0.

Simba SC; iliwakilishwa na Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Shomary Kapombe, Juma Nyosso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi ‘Boban’, Daniel Akuffo, Mrisho Ngassa na Emanuel Okwi.

Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza Azam imelazimishwa sare ya 2-2 na wenyeji Toto African, Uwanja wa Kaitaba Bukoba, wenyeji Kagera Sugar wametoka sare ya bila kufunga na JKT Oljoro ya Arusha, wakati Uwanja wa Sokoine Mbeya, wenyeji Prisons wametoka sare ya 1-1 na Coastal Union ya Tanga na kwenye Uwanja wa Chamazi, African Lyon imeifunga Polisi Morogoro 1-0, wakati Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Ruvu Shooting imeifunga 2-1 Mgambo

MSIMAMO WA LIGI KUU BARA
                           P    W  D   L    GF       GA      GD      P
Simba SC            2    2    -     -     5          -           5          6
Mtibwa Sugar      2    1    1    -     3          -           3          4
Azam FC             2    1    1    -     2          1          1          4
Coastal               2    1    1    -     2          1          1          4
Ruvu Shooting    2    1    -     1    3          3          -           3
JKT Ruvu            2    1    -     1    2          3          -1        3
African Lyon        2    1    -     1    1          3          -2        3
Toto African         2    -     2    1    3          2          1          2
JKT Oljoro           2    -     2    1    1          -           -           2
Prisons                2    -     2    -     1          1          -           2
Polisi Moro           2    -     1    1    -           1          -1        1
Kagera Sugar      2    -     1    1    -           1          -1        1
Yanga SC            2    -     1    1    -           3          -3        1
JKT Mgambo       2    -     -     2    1          3          -2        0

MATOKEO MECHI ZOTE LEO:
JKT Ruvu 0-2 Simba SC
Mtibwa Sugar 3-0 Yanga SC
African Lyon 1-0 Polisi Moro
Ruvu Shooting 2-1 Mgambo JKT
Prisons 1-1 Coastal Union
Kagera Sugar 0-0 JKT Oljoro
Toto Africans 2-2 Azam FC

Photo of the day.... LOl

Viongozi wa Yanga, kushoto Mussa Katabaro na Seif Ahmad 'Magari' wakiwa taaban Uwanja wa Jamhuri jana
Hao ni viongozi wa Yanga pichani hapo jana wakiwa hawaamini kinachoondelea kweny eUwanja wa Jamuhuri Moroggoro ambapo vijana hao wa Jangwani walipigwa 3 bila. Magoli ya Mtibwa yalifungw na Dickson Daudi dk ya 11, na Hussein Javu aliyefinga magoli mawili dakika ya 43 na 86. Katika dakika ya 89 Yanga walipata penalty ambayo nayo walikosa kwani mchezaji wao Hamis Kiiza aliipaisha juu. Ama kweli siku ya kufa nyani...

Watani wanawatania walikwenda na magari ya kifahari na kurudi na Bajaji za miguu mitatu (magoli 3).. lol

Yanga kwa msimu huu kwa kweli hawakuanza vizuri ligi kwani mechi yao ya kwanza walilazimishwa suluhu ya bila kufungana na Prison.

Jana vikosi vy Ynaga na Mtibwa viliwakilishwa na hawa..
Yanga SC; Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, , Mbuyu Twite/Kavumbangu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo/Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Said Bahanuzi, Hamisi Kiiza na David Luhende/Stefano Mwasyika.

Mtibwa Sugar; Shaaban Hassan Kado, Malika Ndeule, Issa R Issa, Dickson Daudi, Salvatory Ntebe, Shaaban Nditi, Jamal Mnyate/Babu Seif Ally, Awadh Juma, Hussein Javu, Shaaban Kisiga ‘Malone’ na Vincent Barnabas/Ally Mohamed 'Gaucho'.