Wednesday, September 12, 2012

Maandamano ya Waandishi wa habari katika picha

Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Bw. Neville Meena akizungumza mara baada ya waandishi wa habari kumaliza maadamano yao ya Amani kutoa ujumbe wao kwa jeshi la Polisi kutokana na kupoteza maisha kwa  mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi aliyeuwawa katika vurugu kati ya Polisi na Wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika kijiji cha Nyololo Mkoani Iringa hivi karibuni, Maandamano hayo yalianzia katika ofisi za kituo cha Televisheni ya Chanel Ten ambako marehemu alikuwa mwakilishi wake mkoani Iringa na kuishia katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam hapo jana.

Waandishi wa habari mbalimbali wakitoa dukuduku zao mara baada ya kumalizika kwa maandamano hayoi.

wandishi wa habari Mkongwe Bw Jackton Manyerere akizungumza katika maadamano hayo kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam

Waandishi wa habari mbalimbali wakiwa wamejikusanya katika ofisi za Chanel Ten kabla ya kuanza kwa maandamano hayo.

Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Bw. Neville Meena akitoa ratiba ya njia ambazo maandamano yatapita kabla ya kuanza kwa maandamano hayo wanaofuatia katika picha ni Profesa Rwaitama, Jane Mihanji na Rashid Kejo.

Waandishi wa habari wakiandamana huku wakiwa wamebeba picha ya marehemu Daudi Mwangosi

Maandamano yakiendelea kupitia mitaa kadhaa  jijini Dar es salaam

Hapa yakiwa yamefikia katika barabara ya Morogoro kuelekea Jangwani.

Waandishi wa habari wakiigiza vurugu zilizotokea  mkoani Iringa ambapo Mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi alipoteza maisha katika vurugu hizo.

Mdau Maximilian kutoka kituo cha Televisheni cha Mlimani TV.

Polisi nao hawakubaki nyuma katika kuhakikisha kuwa swala zima la usalama linachukua mkondo wake
Katika Maanadamano hayo yaliyooishia Viwanja vya Jangwani, Waandishi hao walikataa uwepo wa Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Nchimbi ambaye alikuwepo hapo kuyapokea maandamano hayo kwa sababu walizodai kuwa wanampenda mno lakn kwa siku ya jana hawakumuhitaji kwani hakuvaa vazi la wahusika waliokuwepo pale.

No comments:

Post a Comment